What's New?

9:05 PM

Unknown Unknown Author
Title:
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
HOME Mkusanyiko wa zile Stori zilizopewa Headlines kwenye Magazeti ya leo January 6, 2015 Nimekuwekea hapa MTANZANIA Mkazi w...
HOME

Mkusanyiko wa zile Stori zilizopewa Headlines kwenye Magazeti ya leo January 6, 2015 Nimekuwekea hapa

onMTANZANIA
Mkazi wa Kata ya Buhare Manispaa ya Musoma, Helena Paulo mwenye umri wa miaka 21 amejifungua watoto pacha wa kike walioungana kifua na tumbo katika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Mara.
Kutokana na taarifa za watoto hao kusambaa mitaani,wananchi walimiminika hospitalini hapo kushuhudia watoto hao waliozaliwa Januari 4 mwaka huu likiwa ni tukio la pili baada ya lile la kwanza kutokea Agosti 6 mwaka jana.
Akielezea hali ya pacha mkunga wa zamu wa hospitali hiyo Elisifa Makala alisema  walimpokea mjamzito Helena January 3 akiwa mwenye uchungu wa kawaida na kuamua kumpumzisha kusubiri kujifungua kutokana na kutokua na tatizo lolote.
Alisema ilipofika saa 8 usiku alianza kusikia uchungu ambapo alipewa msaada wa kujifungua lakini alishindwa kujifungua kwa njia ya kawaida kutokana na mtoto kutanguliza miguu na kufanyiwa upasuaji ambapo waliwakuta watoto wakiwa wameshikana.
MTANZANIA
Watu 22 wamepandishwa kizimbani katika mahakama ya jiji la Dar es salaam kwa makosa mawili tofauti,likiwemo la kufanya biashara ya kuuza miili yao.
Akisoma shtaka hilo mwedesha mashtaka Ramadhan Kalinga alisema watuhumiwa hao walikamatwa maeneo ya Ubungo na kwamba walikua wakiuza miili yao huku wakijua kufanya hivyo ni kosa kisheria.
Washtakiwa walikana na kurudishwa kutimiza masharti ya dhamana na shauri lao litaendelea tena Januari 13 mwaka huu.
NIPASHE
Zaidi ya wafanyakazi 150 wa Shirika la Usafirishaji Dar es salaam ‘UDA’ wamefukuzwa kazi Desemba mwaka jana.
Msemaji wa Shirika hilo George Maziku alisema wafanyakazi hao wamepunguzwa ikiwa ni moja ya mikakati ya kuimarisha utendaji wa shirika hilo.
Alisema hatua hiyo imechukuliwa baada ya Shirika kugundua kwamba limeajiri wafanyakazi wengi ambao hawana kazi za kufanya.
“Ni kweli Shirika limeamua kupunguza wafanyakazi tangu Disemba30 mwaka jana,lengo ni kuimarisha utendaji kazi na kuongeza ufanisi wa kazi”alisema Maziku.
NIPASHE
Wizara ya fedha imesema hatua za awali zilizoanza kuchukuliwa na Rais Jakaya Kikwete kushughulikia maazimio ya Bunge kuhusu sakata la uchotwaji wa fedha zaidi ya bilioni 300 za akaunti ya Tegeta Escrow zimewezesha wahisani kuanza kutoa misaada waliyokua wameisitisha awali.
Naibu Waziri wa Wizara hiyo Mwigulu Nchemba alisema katika nusu ya mwaka wa kalenda wa fedha kulikua na changamoto nyingi ikiwemo wahisani kusitisha misaada yao kwa Tanzania kusubiri maamuzi yaliyotolewa na Bunge kuhusiana na sakata la Tegeta Escrow.
“Kama Taifa tuanze misingi ya kujitegemea,tumepata fundisho kupanga miradi ya maendeleo halafu unategemea fedha za wahisani ni tatizo,”alisema Nchemba.
Alisema kutegemea wahisani ni tatizo ambalo nchi inabidi kujipanga kuondokana nalo kwani hali hiyo inakwamisha miradi kuchelewa kutekelezwa wahisani wanaposhidwa kuleta fedha kwa wakati.
NIPASHE
Makabidhiano ya miradi ya ujenzi wa miundombinu ya gesi asilia,likiwemo bomba la kusafirishia gesi kutoka Mtwara hadi Dar es salaam kati ya Mkandarasi wa Shirika la Petrol Tanzania TPDC yanatarajia kufanyika Juni mwaka huu,baada ya kukamilika kwa asilimia 100.
Mwenyekiti wa Bodi ya TPDC, Michael Mwanda na Kaimu Meneja mkuu Mhandisi Kapuulya  Musomba,mradi huo ulianzishwa mwaka 2010 mpaka sasa umefikia asilimia 94.
Musomba alisema mradi huo umegharimu dola za Marekani 1.225 ambazo ni zaidi ya trilioni 1.8 ambazo ni za mkopo.
Alisema benki ya Exim ya China imechangia asilimia 95 huku Serikali ya Tanzania ikichangia asilimia tano kati ya fedha hizo.
NIPASHE
Mahakama kuu ya Tanzania imeiandikia barua Wizara ya Maendeleo ya Mifugo na uvuvi kwa ajili ya kurejesha mali ikiwemo meli ya Tawariq na zaidi ya Bilioni mbili za tani 296.3 za samaki kwa raia wawili wa China.
Kwa mujibu wa barua hiyo iliyosajiliwa na msajili wa mahakama Disemba 17 imeitaka Serikali kurejea ahadi,kupitia hati ya kiapo iliyotolewa na Godfrey Nanyaro,Dk Charles Nyanlundana na Katibu mkuu a Wizara hiyo.
Kwa mujibu wa msajili huyo kiapo kinasema endapo washtakiwa hawatakutwa na hatia mahakamani Serikali italipa gharama za samaki waliokutwa nao wa tani 296.3 ndani ya siku 30 tangu kuachiwa na mahakama.
Mbali na barua hiyo mahakama kuu imeambatanisha nakala ya umri ya kuuza samaki hao uliotolewa Desemba 11 na jaji Radhia Sheikh hukumu ya kuwaachia huru mahakama ya rufani na hati ya mkurugenzi wa mashtaka nchini ya kuwafutia mashtaka.
MWANANCHI
Shirikisho la soka Tanzania TFF limepata nguvu kwani linatarajia kupata dola milioni 1.3 sawa na bilioni 2.2 kutoka kwa Shirikisho la soka duniani FIFA pamoja na fedha za kuiandaa timu ya Taifa ya Tanzania kushirikia mshindano ya kombe la dunia mwaka 2018.
Katibu wa FIFA Jerome Valcke alisema Shirikisho hilo limepanga kuwapa wanachama wake bonasi ya bilioni 2.2 ikiwa ni sehemu ya mapato yake iliyoyapata baada ya kombe la dunia la Brazil kumalizika mwaka jana.
Mbali na fedha hizo pia FIFA itatoa milioni 10 kwa kila mwanachama katika kuziandaa timu zao za Taifa kwa ajili ya kombe la dunia.
MWANANCHI
Baadhi ya wanawake wa Kitanzania waliofungwa katika magereza ya China na Hong Kong walishika mimba kama moja ya mbinu za kutumia kupitisha dawa za kulevya bila kugundulika kwenye uwanja wa ndege na mipaka mingine ya kimataifa.
Watanzania wanne walioko katika Magereza ya China na Hong Kong walijifungua watoto kwa nyakati tofauti wakiwa wanatumikia vifungo na wamekiri kuwa walibeba ujauzito kama mbinu ya kuwasaidia kusafirisha dawa hizo bila kukaguliwa.
Watoto wanaozaliwa magerezani baada ya kufikisha mwaka mmoja hupelekwa katika vituo vya watoto yatima na kusomeshwa na Serikali ya China hadi pale wazazi wao watakapomaliza kutumikia adhabu.
Imebainika kuwa watoto wawili wapo katika vituo hivyo,mmoja tayari yupo Tanzania baada ya kurudishwa na bibi yake na mwingine bado yupo gerezani na mama yake.
MWANANCHI
Polisi imewakamata vijana 510 wanaodaiwa kujihusisha na mtandao wa uhalifu maarufu kama Panya Road katika Wilaya za Kinondoni,Ilala na Temeka.
Wazazi na walezi wa watuhumiwa hao wameonywa kutokwenda kwenye vituo walivyohifadhiwa vijana hao hadi polisi watakapojiridhisha na upelelezi.
Januari 2 maeneo mbalimbali ya Jiji yalikumbwa na taharuki kubwa kwa saa 2 baada ya kuwepo  na uvumi wa kuwepo kwa kundi hilo mitaani na kupora mali za watu.
Baada ya tukio hilo Polisi waliendesha msako mkali na kuwakamata vijana 36 wenye rekodi ya kufanya uhalifu.
Jana Kamanda Kova alisema watuhumiwa wengine 510 walikamatwa katika maeneo mbalimbali ya vijiweni na wengine wakifuatwa katika nyumba wanazoishi baada ya polisi kupata taarifa za kiintelijensia.
06 Jan 2015

About Author

Advertisement

Chapisha Maoni

Emoticon
:) :)) ;(( :-) =)) ;( ;-( :d :-d @-) :p :o :>) (o) [-( :-? (p) :-s (m) 8-) :-t :-b b-( :-# =p~ $-) (b) (f) x-) (k) (h) (c) cheer
Click to see the code!
To insert emoticon you must added at least one space before the code.

 
Top